About us

Tuesday, December 8, 2015

Baseball Tournament is ON in Dar Es Salaam This Week..

Nahodha wa Timu ya Baseball ya Kibasila Pius Peter (kulia) akiwaonyesha waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam jinsi ya mchezo huo unavyochezwa. Kushoto ni Nahodha wa Timu ya Baseball ya Tigers Mussa Mbugi.
Nahodha wa Timu ya Baseball ya Kibasila Pius Peter (wa pili kulia ) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu Mashindano ya Kitaifa ya Awamu ya Tatu ya Mchezo wa Baseball yanayotarajia kuanza Ijumaa ya wiki hii jijini Dar es salaam . Wengine Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Baseball nchini Alpherio Nchimbi(kushoto) ,Nahodha wa Timu ya Baseball ya Tigers Mussa Mbugi( wa pili kushoto) na Nahodha wa Timu ya Baseball ya Giants Douglas Stanslaus.(kulia).

Na Nyakongo Manyama- MAELEZO.


MASHINDANO ya Kitaifa ya Awamu ya Tatu ya Mchezo wa Baseball yanatarajiwa kuanza Ijumaa ya wiki hii jijini Dar es salaam.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Baseball nchini Alpherio Nchimbi leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Amesema kuwa mashindano yatashirikisha timu tisa kutoka Tanzania bara na Visiwani na yanatarajiwa kufunguliwa na Balozi wa Japani nchini Tanzania Mhe. Masaharu Yoshida.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo , mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika katika shule ya Sekondari ya Azania iliyopo jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa mashindano hayo yanayojulikana kama 3rd Koshien Tanzania National Championship yatafanyika kwa muda wa siku tatu kuanza tarehe 11 hadi 13 mwezi huu.

Nchimbi amezitaja timu zitakazoshiriki kuwa ni Shule za Sekondari ya Azania, Kibasila , Iyunga, Sanya Juu, Londoni , na Mwanza Baseball Club, Mwanakwerekwe “C” , Tigers na Giants.




Amesema kuwa mshindano ya mwaka huu yanatarajiwa kusimamiwa na wataalamu kutoka nchini Japan wakishirikiana na wataalam kutoka nchini katika kutoa uamuzi na masuala mengine ya kiufundi.

Nchimbi amesema lengo la mashindano hayo ni kupata timu ya Taifa ya umri wa chini ya miaka 21 kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kushiriki mashindano yatakayofanyika Afrika kusini hapo mwezi wa pili(February ) mwakani (2016).
Kwa upande wa Nahodha wa Timu ya Giants Douglas Stanslaus ametoa wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi kwa ajili kuona mashindano hayo na kuwatia moyo ili waweze kukuza mchezo huo nchini.
Naye Nahodha kwa timu ya Kibasila Pius Peter amewaomba vijana wengi kujitokeza kuona na kujifunza jinsi mchezo huo unavyochezwa ili hatimaye mchezo huo umeweze kuenea sehemu mbalimbali nchini kama fursa ya vijana kushirikiana na kujenga umoja.
Aidha Katibu Mkuu wa Katibu wa Chama cha Mchezo wa Baseball nchini Nchimbi amewaomba wadau mbalimbali kuthamini mchezo wa Baseball kama ilivyo michezo mingine na kujitokeza kuufadhili ili uweze kukua na kutengeneza ajira kwa vijana.

ADS

ADS

ADVATISE HERE

ADVATISE HERE